MAANA YA U.T.I
U.T.I kirefu chake ni
URINARY TRACK INFECTION au kwa lugha nyepesi tunaweza kusema ni maambukizi kwa
njia ya mkojo.
Ugonjwa huu husababishwa
na bakteria anayeitwa Escherichia coli (E. coli) ambao makazi yao ya kawaida ni
kwenye utumbo mpana, hivyo huwa wanapatikana pia kwenye haja kubwa. Lakini
baadhi ya watu wanaweza kupata tatizo hili kutokana na kuingiwa na fangasi ingawa
pia zipo sababu nyingine chache.
Bakteria wa Escherichia
coli hawasababishi peke U.T.I bali huambatana na wengine waitwao
staphylococcus, saprophyti cus, pseudom onas, enterobacter na kadhalika na
maambukizi katika njia ya mkojo mara zote yanatokea kwenye njia ya mkojo na si
pengine popote.
VYANZO VYA U.T.I
1.Maji machafu,matumizi ya maji machafu wakati wa kujisafisha huweza kuweka bacteria kwa urahisi na kusababisha U.T.I
1.Maji machafu,matumizi ya maji machafu wakati wa kujisafisha huweza kuweka bacteria kwa urahisi na kusababisha U.T.I
2.Vyoo kuwa vichafu,pia matumizi ya vyoo ambavyo ni vichafu huweza kusababisha kupata U.T.I kwa sababu ndani ya choo kuna bakteria wengi amabao sababisha U.T.I.
3.Ngono,kufanya ngono mara kwa mara ni tatizo kubwa ambalo huweza kusababisha U.T.I sababu wakati wa ngono msuguano hua mkubwa ambao hufanya bacteria kutoka kupitia maji maji ya ukeni na kuingia katika njia ya mkojo,mtu ambae anafanya ngono mara kwa mara yuko kwenye hatari ya kupata U.T.I kuliko yule ambae hafanyi ngono mara kwa mara.
4.Kuvaa nguo za mitumba
bila kufua, matumizi ya nguo za mtumba bila kufua husababisha kwa urahisi
kupata U.T.I sababu ya bakteria waliomo kwenye nguo hizo.
6.Kemikali, hili ndo tatizo kubwa hasa kwa wanawake wengi ambao siku hizi utumia saana kemikali hasa kwenye vipodozi ambapo kemikali hizi kwa kuwa ni sumu huenda hadi kwenye kibofu na kuchubua kibofu na kua chanzo cha U.T.I
7.Kubana mkojo kwa muda mrefu,pia kubana mkojo kwa muda mrefu kunaweza sababisha U.T.I.
KINGA ZIDI YA U.T.I
Kwa Wanawake, wanashauriwa kuepuka
kujisafisha sehemu za siri na maji machafu na yasiyo salama, pia kuepeuka
kupaka marashi sehemu hizo, ama kutumia pamba zenye kemikali ya kukata harufu
kwani hizo huua bakteria wa asili wa ukeni hali ambayo hukaribisha bakteria wa
maradhi kuzaliana kwa wingi. Pia wanashauriwa wanapojisafisha baada ya
kujisaidia kuanzia mbele kwenda nyuma, ili kuepusha kuhamisha bakteria walio
eneo la haja kubwa na kuingia njia ya mkojo.
Kwa ujumla, unaweza kuudhibiti au
kuponya ugonjwa huu kwa kunywa maji mengi pamoja na juisi itokanayo na matunda
halisi, iwapo tutawahi kabla tatizo halijawa sugu. Kwa maana nyingine, unaweza
kujikinga na ugonjwa huu kwa kuwa na mazoea ya kunywa maji ya kutosha kila
siku. Ukinywa maji ya kutosha yatakufanya uende haja ndogo kila mara na kwa
njia hiyo wale bakteria watakuwa wakitoka na hatimaye kuisha kabisa.
DALILI ZA U.T.I
1.Mwili kuchoka mara kwa mara
1.Mwili kuchoka mara kwa mara
2.Homa ya mara kwa mara
3.Kichwa kuuma mara kwa
mara
4.Kubanwa na mkojo halafu ukienda kukojoa unakuta mkojo kidogo
5.Maumivu wakati wa kukojoa hasa kipindi cha kumalizia mkojo
6.Kiuno kuuma.
4.Kubanwa na mkojo halafu ukienda kukojoa unakuta mkojo kidogo
5.Maumivu wakati wa kukojoa hasa kipindi cha kumalizia mkojo
6.Kiuno kuuma.
MATIBABU YA U.T.I
Matibabu
ufanyika mara baada ya kufanyiwa vipimo na kuthibitika kuwa mgonjwa ana
maambukizi ya U.T.I. Dawa ambazo anaweza kupewa ni kama vile Ciprofloxacin, Monurol, Furadantin,
Sulfam ethoxazole, co-trimax, ampicillin, gentamicin na kadhalika. Mgonjwa anayesumbuliwa
na U.T.I hapaswi kutumia dawa yoyote bila kwanza kupata ushauri wa daktari.
MADHARA YA U.T.I
Kwa wanaume, maambukizi haya huathiri nguvu za kiume maana bakteria
hujipenyeza hadi katika korodani na huathiri uzalishaji wa mbegu za kiume
na kunaweza hata kusababisha ugumba. Hivyo unashauriwa kuhakikisha unatibu bila
kuchelewa ugonjwa huu.
Pia maambukizi ya njia ya
mkojo huweza kusababisha matatizo ya tezi ya kiume (prostate) kwani husababisha
mrija wa mkojo kuziba, kutopitisha mkojo vizuri na kuruhusu bakteria kujenga
makazi. Hali hiyo ikitokea mgonjwa lazima akamuone daktari ili awekewe mrija wa
kutolea mkojo.
MWISHO
Afya ya mwili ni kitu cha
muhimu sana maana kinachangia katika ufanisi wa uzalishaji mali na maendeleo
katika jamii, hivyo sote tunatakiwa kujali afya zetu kwa kufanya mazoezi, kula
vizuri na kunywa maji ya kutosha, kupata muda mzuri wa kupumzika na ata wakati
wa kulala pia kufanya shuguli zetu za maendeleo katika sehemu salama.
0 comments:
Post a Comment