9 Oct 2015

TIZAMA NAMNA WACHIMBAJI WADOGO WA DHAHABU WA NYANGARATA KAHAMA WALIVYO NUSURIKA KUFA BAADA YA MGODI KUPOROMOKA.

Mgodi wa wachimbaji wadogo wa nyangarata wilayani kahama, ulioporomoka.

Watu kumi na moja wamenusurika kifo na wengine zaidi ya saba wanahofiwa
kufa baada ya mgodi wa wachimbaji wadogo wa dhahabu wa Nyangarata wilayani Kahama Shinyanga kuporomoka na kifusi kuwafukia huku wachimbaji waliobaki wakidai kukosa msaada wa kuwaokoa wenzao walioko ardhini wakiomba msaada.

Wakizungumza na waandishi wa habari, baadhi ya wachimbaji katika mgodi huo wameilalamikia serikali kuwatelekeza bila msaada wowote huku wakidai kuwa hata uongozi wa mgodi umeshindwa kuchukua hatua ili kuwaokoa wenzao waliofukiwa na kifusi.

Kwa upande wake katibu mtendaji wa wachimbaji wadogo wilaya ya Kahama amekiri kutokea kwa maporomoko hayo huku akidai kuwa tukio hilo limekua la kutatanisha kwakuwa wakati linatokea watu walikuwa wakifanya kazi zao kama kawaida na wanaohofiwa kufa kati yao wapo wataalamu wa uokoaji wanne wakiokuwa wakijitahidi kuwaokoa wachimbaji hao.

Source: ITV


0 comments:

Post a Comment