20 Sept 2015

THE SOURCE OF MOVEMENT OF SYRIAN PEOPLE TOWARD EUROPEAN COUNTRIES ( Zijue sababu za watu wa syria kukimbilia nchi za ulaya na kua wakimbizi)

Kamati ya kutafuta ukweli ya Umoja wa Mataifa kuhusu Syria imetangaza katika ripoti yake iliyotolewa Alkhamisi tarehe 3 Septemba kwamba Syria inasumbuliwa na mgogoro unaotokana na maslahi ya kijiografia ya madola ya kigeni. Ripoti hiyo imesema kuwa: Vita vya Syria vilianzishwa kwa ajili ya kudhamini maslahi ya baadhi ya nchi za kanda hiyo na za kimataifa.
Hapana shaka kuwa, kifungu hiki cha ripoti ya kamati ya kutafuta ukweli ya Umoja wa Mataifa kuhusu vita vya ndani nchini Syria kinaashiria Marekani, nchi za Ulaya na washirika wao wa Mashariki ya Kati kama Saudi Arabia, Qatar, Uturuki na utawala haramu wa Israel. Ripoti hiyo ya kamati ya Umoja wa Mataifa ambayo imetayarishwa kwa kutegemea mahojiano 355, nyaraka za kitiba, picha za satalaiti na jinai kubwa kama za mauaji, ubakaji, kutekwa nyara watu na uharibifu mkubwa uliofanyika nchini Syria katika kipindi cha miezi sita ya kuanzia Januari mwaka huu, imeitaka jamii ya kimataifa kuwapokea wakimbizi wa Syria na kuzuia maafa makubwa zaidi ya kibinadamu katika nchi hiyo.
Tangu mwaka 2011 Syria ilitumbukizwa katika vita vinavyoendeshwa na nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani. Wasyria ambao wanataabika kutokana na vita hivyo wanalazimika kuwa wakimbizi nchini mwao au kukimbilia katika nchi jirani na barani Ulaya. Inaripotiwa kuwa katika mwaka huu wa 2015 pekee zaidi ya Wasyria 2500 wamefariki dunia katika maji ya Bahari ya Mediterania wakikimbia ukatili wa makundi ya kigaidi kama Daesh. Maiti za wakimbizi hao zinazoopolewa baharini au kuokotwa katika pwani ya nchi kama Uturuki zimewatia simanzi na huzuni watu wengi duniani. Kamisheni Kuu ya Wakimbizi ya Umoja wa Mataifa inakadiria kuwa Wasyria zaidi ya milioni nne wamekimbia nchi yao na imetahadharisha kuhusu maafa makubwa yanayotokea nchini humo.
Hapana shaka kuwa, mgogoro wa Syria ndio mbaya zaidi wa kibinadamu katika karne hii ya 21 na kwa mujibu wa Kamisheni Kuu ya Wakimbizi ya Umoja wa Mataifa, dunia haijawahi kukumbana na mgogoro mkubwa na mbaya kama huu katika kipindi cha miaka 25 iliyopita. Ripoti zinasema kuwa, nusu ya wakazi wote wa Syria wamepoteza makazi yao katika kipindi cha miaka 4 iliyopita na wengi miongoni mwao wamelazimika kuishi ukimbizini.
Zaidi ni kwamba vita hivyo vilivyopangwa na nchi za Magharibi vimezaa matunda mabaya zaidi na wanaharamu makatili kama makundi ya kigaidi ya Daesh na Jabhatu Nusra, mauaji ya kizazi na kuharibiwa turathi za Syria zenye umri wa maelfu ya miaka.
Utumiaji wa silaha zilizopigwa marufuku unaoshuhudiwa Syria kama gesi ya haradali na mabomu ya kemikali umesababisha maafa makubwa sana ambayo yatakuwa na taathira mbaya kwa Syria na kanda nzima ya Mashariki ya Kati kwa miaka mingi hata baada ya nchi hiyo kurejea katika hali yake ya kawaida.  
Wakati huo huo kimya cha jamii ya kimataifa na kutowajibika Umoja wa Mataifa kumezidisha mgogoro wa Syria na ripoti ya kamati ya kutafuta ukweli iliyoundwa kufuatilia suala hilo imethibitisha uhakika huo. 
 
Tokeo la picha la wakimbizi kutoka syria
Baadhi ya wakimbizi kutoka syria wakiwa na mizigo yao

  
Namna uaribifu unavyo tokea uko syria.
source; iranSwhiliRadio (IRIB World Services)



0 comments:

Post a Comment