18 Aug 2016

BW.HARUSI AINGIA MITINI, BI HARUSI AENDELEZA SHEREHE KAMA KAWA, CHEKI STORI NZIMA.

Tukio hilo la aina yake limetokea jumamosi iliyopita katika kanisa katoliki palokia ya Mtakatifu Kaloli Lwaga baada ya bwanarusi kushindwa kufika kanisani kwajili ya kufunga ndoa hali iliyoleta sintofahamu kwa familia ya bibi harusi.
Bwana harusi huyo anajulikana kwajina la Pawa Stephano ambaye alitoa mahari ya kiasi cha shilingi za kitanzania milioni moja licha ya kutoonekana siku ya harusi.
Baada ya tukio hilo kutokea familia ya bibi harusi iliendelea na sherehe ya kumpongeza binti yao huku baadhi ya ndugu jamaa na marafiki wa upande wa bwana harusi waliokua wamealikwa wakiuzuria bila tabu.
Paroko wa Parokia hiyo alisema yeye ndie alietakiwa kubariki ndoa iyo siku hiyo na maharusi ao walipata mafundisho ya ndoa na sheria zake.

0 comments:

Post a Comment