Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha ametangaza kufuta matokeo ya Uchaguzi Zanzibar, uliofanyika Oktoba 25, 2015.
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha
Jecha amesema kuwa, ZEC imefuta matokeo ya uchaguzi kutokana na kukiukwa kwa sheria na taratibu mbalimbali za uchaguzi wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo.
Uchaguzi huo utarudiwa baada ya siku 90.
NA HII HAPA CHINI NDIO TAARIFA KWA UMA TOKA ZEC
Na Muda mchache baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salim, kutangaza kuufuta uchaguzi mkuu wa 2015, makamishna wawili wa Tume hiyo, Ayoub Bakar na Nassor Khamis, wameuita uamuzi huo kuwa "si wa ZEC, bali wa Jecha binafsi" na wamejitenga mbali nao.
Ayoub Bakar
Nassor Khamis
0 comments:
Post a Comment