8 Dec 2015

HIZI NDIZO ADA ELEKEZI TOKA SERIKALINI KWA SHULE BINAFSI, ZITAZAME HAPA,WAZAZI MSHINDWE NYINYI TU KUSOMESHA.



Taharuki imetanda kwa wamiliki wa shule nchini baada ya kupokea waraka unaowakataza kuongeza ada kwa shule zisizo za serikali katika mwaka wa masomo unaoanza mwezi ujao.

Kwa mujibu wa tangazo hilo lililotolewa Desemba 3, mwaka huu na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Sifuni Mchome, shule zinatakiwa kutoongeza ada mwaka wa masomo 2016 hadi zitakapopata maelekezo kutoka kwa Kamishna wa Elimu.

Tangazo hilo pia lilieleza kuwa kwa shule ambazo zimeongeza ada bila kupata kibali cha Wizara, kamwe hazitatambuliwa kwani ni batili na kwamba zimefutwa kwavile hazina nguvu kisheria.

Kadhalika, tangazo hilo lilieleza kuwa ada zote kwa shule zisizo za serikali zitabaki kama zilivyoidhishwa na kamishna ambapo waraka wa Elimu Na. 4 wa mwaka 2008 umeelekeza ada zinazotozwa shule za msingi na sekondari pamoja na zisizo za serikali.
Ada iliyowekwa kwa shule za kutwa zisizo za serikali ni Sh. 150,000 na shule za bweni Sh. 380,000 kwa mwaka kila mwanafunzi.

Source: IPP MEDIA.COM

0 comments:

Post a Comment